Singida FG yashusha kocha Mjerumani

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st September 2023


Singida FG yashusha kocha Mjerumani

Baada ya kutangaza kuachana na Hans vs Pluijm, klabu ya Singida FC imemtambulisha Ernst Middendorp raia wa Ujerumani kuwa kocha mkuu wa timu hiyo

Rais wa Klabu Singida Fountain Gate Japhet Makau, amesema Middendorp amekuja na kocha msaidizi pamoja na kocha wa utimamu wa mwili (physic), ambao watawasili nchini siku za hivi karibuni

Middendorp amewahi kuvinoa vilabu vya Arminia Bielefeld na VfL Bochum za Bundesliga, Chippa United, Saint George, Kaizer Chiefs, Swallows FC, Maritzburg United na SV Meppen ya Ujerumani


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.