Baada ya kutangaza kuachana na Hans vs Pluijm, klabu ya Singida FC imemtambulisha Ernst Middendorp raia wa Ujerumani kuwa kocha mkuu wa timu hiyo
Rais wa Klabu Singida Fountain Gate Japhet Makau, amesema Middendorp amekuja na kocha msaidizi pamoja na kocha wa utimamu wa mwili (physic), ambao watawasili nchini siku za hivi karibuni
Middendorp amewahi kuvinoa vilabu vya Arminia Bielefeld na VfL Bochum za Bundesliga, Chippa United, Saint George, Kaizer Chiefs, Swallows FC, Maritzburg United na SV Meppen ya Ujerumani



