Droo ya michuano ya kwanza barani Afrika inayokutanisha vigogo African Football League imefanyika leo nchini Misri ambapo Wekundu wa Msimbazi Simba watachuana na mabingwa wa soka Afrika, Al Ahly
Mchezo wa ufunguzi utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, Oktoba 20 Simba ikiwa mwenyeji na mchezo wa marudiano kupigwa Oktoba 24 huko Misri
Michezo mingine, Enyimba watachuana na Wydad Athletic wakati TP Mazembe watachuana na Esperance
Mchezo wa nne wa robo fainali ni kati Petro Atletico dhidi ya Mamelodi Sundowns
Mshindi wa mchezo kati ya Simba dhidi ya Al Ahly atakutana na mshindi wa mchezo kati ya Petro Atletico dhidi ya Mamelod Sundows