Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu Septemba 04 2023

Joel JJ By Joel JJ
4 Sep 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu Septemba 04 2023

Nahodha wa zamani wa Uhispania Sergio Ramos, 37, amepiga hatua katika mazungumzo ya kurejea kwake Sevilla miaka 18 baada ya kuondoka katika klabu hiyo na kujiunga na Real Madrid. Beki huyo aliondoka Paris St-Germain msimu huu wa joto wakati mkataba wake ulipomalizika. (ESPN)

Kakake Joao Palhinha anasema uhamisho wa kiungo wa Ureno na Fulham kwenda Bayern Munich "uliahirishwa", baada ya mazungumzo kuvunjika siku ya mawisho ya uhamisho wa wachezaji. (Mail)

Chelsea ilitoa nafasi kwa Tottenham kumsajili kiungo wa kati wa England James Maddison, 26, msimu wa joto kwa sababu hakuendana na wasifu wa umri wa walengwa wao wa uhamisho. (Football Insider)

Kipa wa zamani wa Manchester United na Uhispania David de Gea, 32, ni miongoni mwa wachezaji kadhaa wanaopatikana kwa uhamisho wa bure ambao unavutia klabu za Saudia. (Marca kwa Kihispania)

Winga wa Atletico Madrid na Ubelgiji Yannick Carrasco, 29, anatazamiwa kuhamia Al Shabab ya Saudia kwa £12.8m. (ESPN)

Matumaini ya meneja Wayne Rooney kuwasajili tena kiungo wa Jamaica Ravel Morrison, 30, kiungo wa kati wa Uingereza Jesse Lingard, 30, na mshambuliaji wa Ghana Andre Ayew, 33, ambao wote ni wachezaji huru, yamezimwa na masuala ya mishahara katika klabu ya MLS DC United. (Washington Post - usajili unahitajika)

Klabu ya Monaco ya Ligue 1 inapanga kumsajili beki wa Fulham Muingereza Tosin Adarabioyo, 25, mwezi Januari baada ya kujitahidi sana kufanikisha dili lake katika uhamisho wa msimu wa kiangazi. (Fabrizio Romano)

Barcelona hawajafurahishwa na majaribio ya Manchester City kumsajili beki wa kushoto wa Uhispania Alejandro Balde, 19, winga aliyeitwa Lamine Yamal, 16 na mchezaji wa kimataifa wa Uhispania Pau Cubarsi, 16, msimu huu. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Beki wa Chelsea na Brazil Thiago Silva, 38, alizozana na mashabiki kwenye Instagram baada ya klabu hiyo kushindwa na Nottingham Forest katika mechi ya Ligi ya Premia na siku ya Jumamosi. (Telegraph - usajili unahitajika)

BBC

More Stories

Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
57m ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
1h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
3h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
13h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
13h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
14h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
17h ago
READ MORE →