Yanga - Local

Maxi apania kuibeba Yanga Kimataifa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Sep 2023
Maxi apania kuibeba Yanga Kimataifa

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Maxi Mpia Nzegeli ameweka wazi kuwa malengo yake ni kuhakikisha kuwa anaisaidia timu hiyo kufanya vyema katika michuano ya kimataifa na kufikia malengo yao ya kufika hatua ya makundi

Yanga ili wafanikiwe kutinga katika hatua ya makundi wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanawaondoa Al Merrikh katka mchezo unaofuata wa hatua ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika

Maxi amesema kuwa malengo yake ni kuhakikisha anaisaidia Yanga kufika kwenye malengo kwenye michuano hiyo kwa kufika katika hatua ya makundi huku akiamini kuwa wana uwezo mkubwa wa kuwaondoa Al Merrikh

"Malengo ya timu ndio malengo ya wachezaji wote, kwetu sisi tunatamani kuona tukifika katika makundi na kupita zaidi ya hapo, kikubwa kwetu tunachokifanya kwa sasa ni kuona tunajikita zaidi katika kufanya vyema katika michezo yetu"

"Michezo yetu miwili iliyopo mbeleni dhidi ya Al Merrikh ni muhimu zaidi kwa upande wetu kuona tunafanya vyema na kupata matokeo, tunaamini tunao uwezo huo na tutapambana zaidi kufikia hayo malengo," alisema

Maxi amekuwa na mwanzo mzuri katika kikosi cha Yanga akifunga mabao mawili, kutoa pasi moja ya bao kwenye mechi ya hatua ya awali ligi ya mabingwa dhidi ya Asas Fc

Maxi pia amefunga mabao mawili na kutoa pasi moja ya bao katika mechi mbili alizocheza kwenye ligi kuu ya NBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
36m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’