Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Septemba 07 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th September 2023


Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Septemba 07 2023

Klabu ya Al-Ittihad ya Saudi Arabia iko tayari kuwasilisha dau la pauni milioni 200 kumnunua nyota wa Liverpool kutoka Misri Mohamed Salah, 31, lakini inahofia muda unayoyoma, leo Alhamisi ndio siku mwisho ya uhamisho wa wachezaji. (Telegraph - usajili unahitajika)

Beki wa zamani wa Uingereza na Chelsea John Terry, 42, yuko mbioni kujiunga na Al-Shabab FC ya Saudia kufanya mafanikio yake ya usimamizi. (Sun)

Kipa wa Tottenham Hugo Lloris, 36, huenda akasalia nje ya uwanja hadi Januari huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa akiwa hajaonyesha nia ya kuondoka licha ya Spurs kupokea ofa kadhaa. (Guardian)

Beki wa Tottenham na Uingereza Eric Dier amefanya mazungumzo na mwenyekiti Daniel Levy baada ya kufungiwa na kocha Ange Postecoglou. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 amekuwa akihusishwa na uhamisho wa kwenda Saudi Arabia. (Telegraph - usajili unahitajika)

Liverpool ilijaribu kumsajili mshambuliaji wa Uruguay Darwin Nunez, 24, badala ya Joao Felix kabla ya mshambuliaji huyo wa Ureno, 23, kujiunga na Barcelona kutoka Atletico Madrid. (Mundo Deportivo)

Bayern Munich wanatazamia kuwasilisha ofa mpya kwa kiungo wa Fulham Mreno Joao Palhinha, 28, mwezi Januari. (Standard)

Nahodha wa zamani wa Manchester City lkay Gundogan, 32, amekiri kwamba alipuuza nia ya Arsenal na klabu zingine msimu huu kwa sababu kuichezea Barcelona ilikuwa "ndoto ya utotoni" ya kiungo huyo wa Kijerumani. (Mirror)

Beki wa Chelsea Muingereza Levi Colwill, 20, amefichua kuwa mchezaji-mwenza wa zamani wa Brighton na nyota wa zamani wa Liverpool Adam Lallana alimshawishi kusaini mkataba mpya na kusalia Stamford Bridge chini ya kocha Mauricio Pochettino. (Mail)

Mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 32, yuko tayari kuondoka Atletico Madrid mwisho wa msimu huu na kujiunga Lionel Messi katika Ligi Kuu ya Soka ya Marekani. (Sport, via Mail)

Chelsea walifanya mazungumzo na shirika la ndege la serikali ya Saudia Riyadh Air juu ya kuwa mfadhili mpyawa klabu hiyo. (Times - usajili unahitajika)

Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, yuko tayari kuachana na nyongeza ya uaminifu ya pauni milioni 68.6 katika mkataba wake wa Paris St-Germain, lakini amesisitiza kwamba hatasaini mkataba mpya. (90min)

Nyota wa zamani wa Real Madrid na Chelsea Eden Hazard, 32, amedokeza kwamba anakaribia kustaafu katika makala maalum kuhusu timu ya taifa ya Ubelgiji. (Mail)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.