Spain - Local

Busu lilivyomponza rais wa soka Hispania

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Sep 2023
Busu lilivyomponza rais wa soka Hispania

Rais wa Shirikisho la Soka Hispania, Luis Rubiales ametangaza kujiuzulu katika nafasi yake baada ya kuandamwa na tuhuma za unyanyasaji wa kijinsia baada ya kumbusu mdomoni mshambuliaji wa timu ya wanawake ya nchi hiyo, Jenni Hermoso

Hermoso (33) alisema busu alilopigwa na Rais huyo halikuwa la maafikiano wala makubaliano kati yao na tayari alishawasilisha madai ya kisheria

Rubiales alikumbwa na tuhuma hiyo siku ya fainali ya Kombe la Dunia la Wanawake baada ya ushindi wa Hispania dhidi ya Uingereza

Kwa upande wake Rubiales alisema amewasilisha kujiuzulu kwake kwa Kaimu Rais wa shirikisho hilo

Aidha, Rubiales pia amejiuzulu wadhifa wake kama Makamu wa Rais wa Kamati Kuu ya Uefa

Siku ya Ijumaa, mwendesha mashtaka aliwasilisha malalamiko katika mahakama kuu ya Hispania kufuatia ushahidi wa Hermoso siku ya Jumanne dhidi ya Rubiales kwa unyanyasaji wa kijinsia na kulazimishwa

Wachezaji 81 wanawake Hispania, wakiwemo washindi wote 23 wa Kombe la Dunia, walisema hawataichezea tena timu ya Taifa kama bado Rubiales atakuwa kwenye nafasi yake.

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
5m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
34m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’