Bodi ya Ligi yapangia tarehe viporo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th September 2023


Bodi ya Ligi yapangia tarehe viporo

Bodi ya Ligi Kuu imeipangia tarehe michezo ambayo ilisogezwa mbele kupisha kalenda ya mashindano ya CAF na FIFA

Kulingana na taarifa iliyotolewa na TFF mapema leo, mchezo kati ya Yanga dhidi ya Namungo Fc utapigwa Septemba 20 katika uwanja wa Azam COmplex

Mchezo kati ya Simba dhidi ya Coastal Union utapigwa Septemba 21 katika uwanja wa Uhuru wakati pia mchezo kati ya Azam Fc dhidi ya Singida FG nao ukipigwa katika uwanja wa Azam Complex

Hata hivyo tarehe hizo zinaweza kubadilika kama CAF itathibitisha uwepo wa mechi za mashindano ya CHAN yanayohusisha wachezaji wa ndani

Kulingana na kalenda ya CAF, mechi hizo zinapaswa kuanza mwishoni mwa mwezi Septemba 2023


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.