Niyonzima aitabiria Yanga ushindi Rwanda

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th September 2023


Niyonzima aitabiria Yanga ushindi Rwanda

Kiungo wa kimataifa wa Rwanda ambaye amewahi kukipiga ndani ya timu za Simba na Yanga, Haruna Niyonzima, amesema mbali na mapokezi makubwa ambayo kikosi cha Yanga itayapata itakapotua nchini Rwanda, pia anaamini timu hiyo ina uwezo mkubwa wa kuifunga Al Merrikh. Septemba 16

Yanga wanatarajiwa kuvaana na Al Merrikhya Sudan, katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa hatua ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika utakaochezwa nchini Rwanda kusaka tiketi ya kufuzu hatua ya makundi

Kwa vipindi vitatu tofauti, Niyonzima amewahi kuhudumu katika timu za Simba na Yanga, huku akifanikiwa kushinda makombe matano ya Ligi Kuu Bara ndani ya misimu mitatu mfululizo. Akizungumzia mchezo huo, amesema amefurahi kuona Yanga ikirejea kucheza Rwanda

"Nafurahi kuona timu yangu ya Yanga inakuja hapa Rwanda kwa ajili ya mchezo wa kimataifa dhidi ya Al Merrikh, napenda kuwaahidi kuwa nitakuwa mstari wa mbele kuongoza mapokezi, lakini pia kuhakikisha Yanga inapata matokeo ya ushindi na kuondoka hapa wakiwa na tabasamu," alisema Niyonzima


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.