Tetesi za soka Ulaya, Jumapili Septemba 17 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th September 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumapili Septemba 17 2023

Barcelona wana nia ya kutaka kumnunua winga wa Manchester United na England Jadon Sancho, 23, licha ya masaibu yanayomkumba Old Trafford. (Sport - kwa Kihispania)

Kiungo wa Arsenal na Ghana Thomas Partey, 30, huenda akauzwa mwezi Januari huku Juventus ikitarajiwa kuwa kituo chake. (Football Insider)

Sheffield United inapania kumnunua kocha wa zamani Chris Wilder kama mbadala wa Paul Heckingbottom, baada ya kushindwa na Tottenham siku ya Jumamosi. (Mail)

Arsenal wanakaribia kuafiki mkataba mpya wa miaka minne na kiungo wa kati wa Norway Martin Odegaard, 24, wenye thamani ya zaidi ya £200,000 kwa wiki. (Football Insider)

Mshambuliaji wa Ureno Cristiano Ronaldo, 38, anaishtaki klabu yake ya zamani ya Juventus katika harakati ya kutafuta pauni milioni 17 kama mshahara ambao haukulipwa wakati wa janga la Covid-19. (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)

Everton bado wana nia ya kumsajili winga wa Leeds na Italia Wilfried Gnonto, 19, baada ya kushindwa na ofa msimu wa joto. (Football Insider)

Bayern Munich na Real Madrid ziko mbioni kumwajiri kiungo wa kati wa zamani wa Uhispania na mkufunzi wa sasa wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso kama kocha msimu ujao. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Dinamo Zagreb, klabu ya kwanza ya kulipwa ya Luka Modric itajaribu kumnunua tena kiungo huyo wa Croatia, 38, kutoka Real Madrid mwezi Januari. (90 min)

Conor Gallagher kwa sasa anaridhika kuwa Chelsea, ingawa Tottenham wanapanga kurejelea tena azman ya kumnunua kiungo huyo wa Uingereza, 23, mwezi Januari. (Football Insider)

Barcelona bado hawajajadili mpango wa kuongeza mkataba wa mchezaji Frenkie de Jong, 26, huku mkataba wa sasa wa kiungo huyo wa Uholanzi ukitarajiwa kumalizika 2026. (Marca - kwa Kihispania).

Athletic Bilbao wana imani Nico Williams atasaini mkataba mpya, licha ya Barcelona kuonyesha nia ya kumsajili winga huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 21, ambaye mkataba wake unamalizika msimu ujao. (Sport - kwa Kihispania) Liverpool na Manchester United pia wanamtaka Williams. (Football transfers)

Mpango wa 777 Partners wa kuinunua klabu ya soka ya Everton uko mashakani baada ya uchunguzi kuanzishwa kufuatia hoja iliyoibuka kuhusu uwekezaji wa kampuni hiyo katika mpira wa vikapu wa Uingereza. (Telegraph - usajili unahitajika)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.