Mshambuliaji Amissi Tambw ameuandikia barua uongozi wa Singida FG akiupa siku saba ili ukamalishe madai yake kabla hajatimkia Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA) kushtaki
Tambwe alitemwa na Singida FG katika dirisha la usajili lililopita lakini mwenyewe amesema bado ana mkataba wa mwaka mmoja na klabu hiyo
"Bado nina mkataba wa mwaka mmoja na Singida, ila wamenisitishia bila ya mazungumzo na cha kushangaza nalipwa mshahara wangu kila mwezi, lakini madai yangu ya fedha za usajili hayafanyiwi kazi"
"Nimeongea na Mwanasheria wangu ameniambia tayari amewatumia barua kuwaamuru wanilipe fedha yangu ndani ya siku saba tangu aitume barua hiyo na kama watashindwa kufanya hivyo mpango wangu ni kwenda FIFA,"alisema Tambwe
Tambwe amefunguka kuwa baada ya msimu uliopita kumalizika alirudi kwao Burundi kwa mapumziko na muda wa kurudi ulipowadia ili kujiandaa na msimu mpya alizungumza na uongozi juu ya kutumiwa tiketi ya ndege lakini walikuwa wakimuahidi bila utekelezaji, kabla ya kuambiwa hatakuwa tena na timu hiyo
"Sikutumiwa tiketi, ila baadaye tulifanya mazungumzo na nikaambiwa hawatakuwa nami kikosini kwa msimu huu bila sababu yoyote na kukubaliana kunipa madai yangu, lakini hadi sasa hawajafanya hivyo na wamekuwa wakiniingizia mshahara kama kawaida"
"Shida yangu ni kulipwa fedha yangu ya usajili ya msimu mmoja uliobaki ambao naingiziwa mshahara kama makubaliano yetu yalivyokwenda shida ni fedha ya usajili ambayo taarifa yake ipo kwa mwanasheria wangu na ameifanyia kazi kwa kuutaka uongozi kunilipa kama makubaliano yetu yalivyokuwa"



