Singida - Local

Singida FG uso kwa uso dhidi ya Future Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Sep 2023
Singida FG uso kwa uso dhidi ya Future Fc

Achana na matokeo ya mechi za jana za Ligi ya Mabingwa Afrika wakati Simba na Yanga zilipocheza ugenini Zambia na Rwanda, hapa Dar es Salaam leo jioni, Singida Big Stars ina jambo lake kwenye Uwanja wa Azam Complex wakati itakapoikaribisha Future ya Misri katika Kombe la Shirikisho

Mchezo huo utakaopigwa saa 10:00 jioni unazikutanisha timu hizo, huku Singida ikitinga hatua hiyo kwa kuitoa JKU ya visiwani Zanzibar kwa jumla ya mabao 4-3, ilihali wageni wakianzia raundi ya pili ya michuano hiyo inayoendeshwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Kocha mkuu wa Singida inayoshiriki michuano ya CAF kwa mara ya kwanza, Ernst Middendorp akizungumzia mchezo huo alisema lengo ni kupata matokeo mazuri nyumbani ili kupunguza presha mechi ya ugenini ambayo itakuwa ngumu zaidi kwao tofauti na ya mwanzo

"Kwa uzoefu wangu hii michezo ya Afrika kila timu inatengeneza mazingira ya kushinda nyumbani, sasa hii ni fursa kwetu ya kutumia vizuri uwanja wetu kisha kujiandaa na marudiano yatakayoamua hatima yetu," alisema Middendorp

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
15h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
19h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
21h ago
READ MORE β†’