Yanga kuwaenzi waliosafiri Rwanda

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th September 2023


Yanga kuwaenzi waliosafiri Rwanda

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe amewataka Wanachama na Mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc ambao utapigwa Jumatano, Septemba 20 katika uwanja wa Azam Complex

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Kamwe alitangaza kuwa mchezo huo watautumia kuwaenzi mashabiki waliosafiri kwa wingi kwenda Rwanda kuishangilia Yanga kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Al Merrikh ambao Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0

Kamwe alitangaza viingilio vya mchezo huo ambapo VIP A ni Tsh 20,000/-, VIP B ni Tsh 10,000/- na Mzunguuko ni Tsh 5,000/-

"Yanga imekuwa klabu ya kwanza barani Afrika kusafiri na mashabiki wengi katika mechi ya ugenini na kujaza uwanja. Hili ni jambo lililotupa heshima kubwa Afrika nzima na hivyo tumeufanya mchezo dhidi ya Namungo Fc kuwa maalum kwa ajili ya mashabiki waliosafiri Rwanda"

"Tumeandaa utaratibu siku ya Jumatano ambapo itakapofika dakika ya 12 mashabiki wote watasimama na kupiga makofi kwa dakika moja ikiwa ni ishara ya kuwapongeza wote waliosafiri na timu Rwanda"

"Uongozi pia umeandaa surprise kwenye dakika ya 12 ambayo itaonekana uwanjani na Azam Tv kwa wale ambao hawatakuwa uwanjani. Tunawaomba hata wale ambao watakuwa nyumbani au katika vibanda umiza wasimame kwenye dakika ya 12 kuwapa maua yao wale waliosafiri Rwanda," alisema Kamwe


  

More Stories

Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Today, READ MORE β†’
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Today, READ MORE β†’
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Today, READ MORE β†’
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Sowah kurejea Singida BS?
Sowah kurejea Singida BS?
Today, READ MORE β†’
Mubiru atua Azam Fc
Mubiru atua Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Today, READ MORE β†’
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Today, READ MORE β†’
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’