Mashabiki wanne wa klabu ya Namungo Fc wamefariki huku wengine 16 wakijeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea mapema leo mkoani Lindi
Ajali hiyo ilitokea Mitaja karibu na Somanga ambapo mashabiki hao walikuwa wakielekea jijini Dar es salaam kushangilia timu yao katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Yanga ambao utapigwa leo katika uwanja wa Azam Complex

Mwenye ez Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi, Amen..



