Mlinzi kiraka wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Novutus Dismus jana alicheza kwa dakika 90 mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya uliokutanisha timu yake Shakhtar Donestk dhidi ya Porto
Novutus alitumika kama mlinzi wa kushoto na baadae kuhamishiwa safu ya ulinzi wa kati timu yake ikikubali kipigo cha mabao 3-1 nyumbani
Nova anakuwa mchezaji wa tatu mTanzania kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya Kassim Manara na Mbwana Samatta
Shakhtar imepangwa kundi H katika michuano ya ligi ya mabingwa Ulaya ikiwa sambamba na Porto, Antwerp na Fc Barcelona
Mchezo wao utakaofuata kwenye michuano hiyo ni Oktoba 04 ugenini dhidi ya Antwerp



