Yanga imerejea kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya NBC baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Namungo Fc
Yanga ililazimika kusubiri mpaka dakika ya 88 kufunga bao la ushindi liliwekwa kambani na Mudathir Yahya aliyeingia kwenye kipindi cha pili
Mudathir alimalizia krosi ya chini kutoka kwa Yao Yao
Yanga imefikisha alama 9 na mabao 11 ya kufunga na hivyo kuiondoa Mashujaa Fc iliyokuwa kileleni mwa msimamo wa ligi na alama 7





