Hat trik ya pili msimu huu imefungwa na Jean Baleke leo katika mchezo kati ya Simba dhidi ya Coastal Union uliopigwa uwanja wa Uhuru Simba ikiibuka na ushindi wa mabao 3-0
Baleke alifunga hat-trik hiyo katika kipindi cha kwanza akipokea pasi kutoka kwa Clatous Chama, Mohammed Hussein na bao la tatu akifunga kupitia mkwaju wa penati baada ya Luis Miquissone kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari
Coastal Union walicheza pungufu kwa muda mrefu wa mchezo baada ya mshambuliaji wao Hija Ugando kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi Hennock Inonga wa Simba aliyelazimika kukimbizwa Hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi
Pengine Simba ingeweza kufunga mabao mengi zaidi kama wachezaji wake wangekuwa na umakini kwani walitawala mchezo huo na kutengeneza nafasi nyingi
Ushindi huo umeipandisha Simba mpaka nafasi ya pili ikifikisha alama tisa kama ilivyo kwa vinara Yanga ambao wamefunga mabao mengi zaidi



