Crystal Palace wanatarajiwa kuanzisha mazungumzo ya awali kuhusu mkataba mpya na winga wa Uingereza Eberechi Eze, 25, ambaye mkataba wake wa sasa utaendelea hadi 2025. (Athletic - usajili unahitajika)
Manchester United wako tayari kumuuza winga wa Uingereza Jadon Sancho, ambaye walimnunua kwa pauni milioni 73 kutoka Borussia Dortmund, kwa bei iliyopunguzwa Januari. (Star)
Tottenham wanatazamiwa kutekeleza kipengee cha chaguo katika kandarasi ya mshambuliaji wa Korea Kusini Son Heung-min, 31, ambayo itaongeza mkataba wake kwa mwaka zaidi hadi 2026. (Telegraph - usajili unahitajika)
Bayern Munich watachuana na Real Madrid kumsajili nahodha wa Chelsea na beki wa pembeni wa Uingereza Reece James mwaka ujao. (Fichajes - kwa Kihispania)
Beki wa Chelsea Trevoh Chalobah anatazamiwa kuondoka katika klabu hiyo mwezi Januari, huku beki huyo Mwingereza mwenye umri wa miaka 24 akitaka kuhamia Bayern Munich baada ya kukataa Nottingham Forest. (Fabrizio Romano)
Kocha wa Barcelona Xavi amekubali kuongeza mkataba wa mwaka mmoja hadi 2025 katika mkataba ambao una chaguo la kuongezwa kwa miezi 12 zaidi. (ESPN)
Juventus wameungana na Liverpool, Paris St-Germain, Bayern Munich na Tottenham katika mbio za kumsajili kiungo wa kati wa Ufaransa Khephren Thuram mwenye umri wa miaka 22 kutoka Nice. (90 Min)
Arsenal, Chelsea na Manchester United wanavutiwa na winga wa Norway na Club Bruges Antonio Nusa, mwenye umri wa miaka 18 mwenye thamani ya karibu £30m. (Express)
Kocha wa zamani wa Bayern Munich Julian Nagelsmann, 36, anakaribia kufikia makubaliano ya kuwa meneja mpya wa Ujerumani. (Fabrizio Romano)
Liverpool wako tayari kuwasiliana na wawakilishi wa kiungo wa kati wa Uhispania Thiago Alcantara,32, na beki wa Cameroon Joel Matip,32, kujadili mikataba mipya. Mkataba wao unamalizika msimu ujao. (Caught offside)
Mshambulizi wa Ubelgiji Romelu Lukaku alitengana na wawakilishi wa Roc Nation muda mfupi baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 kuhamia Roma kwa mkopo kutoka Chelsea msimu huu. (Telegraph - usajili unahitajika)
Timu kadhaa za Ligi ya Premia, zikiwemo Wolves, Everton na Nottingham Forest ziko tayari kumnunua Michail Antonio ikiwa mshambuliaji huyo wa Jamaica, 33, atashindwa kuafikiana na West Ham kwa mkataba mpya. (Football Insider)
BBC



