Tunakwenda makundi Shirikisho - Kakolanya

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th September 2023


Tunakwenda makundi Shirikisho - Kakolanya

Mlinda lango wa Singida Fountain Gate, Beno Kakolanya amesema licha ya mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Future ya Misri utapigwa ugenini, lakini anaiona nafasi ya timu yao kutinga makundi ya michuano hiyo

Timu hizo zitakutana Oktoba Mosi katika Uwanja wa Al-Salaam, Cairo, Misri, huku Singida ikiwa na faida ya ushindi wa bao 1-0 ilioupata wiki iliyopita Dar

Akizungumzia mchezo wa ugenini, Kakolanya alisema Simba na Yanga zimejiweka pazuri, lakini wao ni ngumu kwa kuwa walianzia nyumbani na ushindi mwembamba. Hata hivyo, kipa huyo alisema ushindi waliopata nyumbani unawapa nguvu ya kutinga makundi na kwamba kila mchezaji atajitolea kuhakikisha wanapata matokeo mazuri

"Tunajua mchezo hautakuwa mwepesi, tunafahamu utamaduni wa timu za waarabu wanapocheza nyumbani. Lakini ushindi tuliopata nyumbani sio haba, tunakwenda kupambana na muhimu ni kuwa na nidhamu," alisema Beno


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.