Tetesi za soka Ulaya, Jumapili Septemba 24 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th September 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumapili Septemba 24 2023

Mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney yuko tayari kuondoka Brentford mwezi Januari. Klabu hiyo iko tayari kuruhusu mchezaji huyo, 27, ambaye anatumikia marufuku ya miezi minane kwa kukiuka sheria za kamari za Shirikisho la Soka, aondoke ikiwa thamani yao ya pauni milioni 60 itafikiwa. (Sunday Mirror)

Arsenal, Tottenham na West Ham zote zinafuatilia uwezekano wa kumnunua winga wa Paris St-Germain na Ufaransa Ousmane Dembele kwa mkopo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alijiunga na mabingwa hao wa Ufaransa msimu wa joto akitokea Barcelona. (Sunday Mirror)

Kiungo wa kati wa Newcastle na Brazil Bruno Guimaraes amekubali kwa mdomo kuongezewa mkataba mpya huku mchezaji huyo, 25 akipanga kuongeza mkataba wake wa sasa hadi 2028. (Sky Sports).

Manchester United ilijaribu kubadilishana wachezaji kadhaa, akiwemo kiungo wa kati wa Uholanzi Donny van de Beek, 26, na kiungo wa kati wa Brazil Fred, 30, kama njia ya kufidia gharama ya kumsajili Rasmus Hojlund. Lakini Atalanta walikuwa wanavutiwa tu na pesa taslimu kwa Dane, 20. (The Athletic - subscription required)

Van de Beek anawindwa na Villarreal baada ya kukosa nyota ya kupendwa na Manchester United. (Fichajes - in Spanish)

United pia wameanza mazungumzo na kiungo wa kati wa Tunisia Hannibal Mejbri, 20, kuhusu mkataba mpya. (Sunday Express) Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy yuko tayari kuuza hisa za hadi 25% katika klabu hiyo. (Sunday Times)

Everton itajaribu kujadili upya masharti ya uhamisho wa kiungo wa kati wa Uingereza Dele Alli, 27 kutoka Tottenham huku Spurs wakitarajiwa kupokea £10m atakaposhiriki mechi zaidi ya 20 za Everton. Lakini hali ya kifedha ya Toffees inaweza kuwalazimisha kufanya mazungumzo. (Sunday Express)

West Brom inaripotiwa kuongeza kasi ya kutafuta mmiliki mpya, huku mfanyabiashara Mchina Guochuan Lai akitaka kuiuza kabla ya mwisho wa mwaka. (Mail on Sunday)

Chelsea na Bayern Munich zimesalia na nia ya kumsajili mlinda lango wa England na Arsenal Aaron Ramsdale, 25, ambaye amepoteza nafasi yake kama nambari moja wa The Gunners. (Mail on Sunday)

Hata hivyo, Ramsdale hayuko katika haraka ya kufanya maamuzi yoyote kuhusu mustakabali wake. (Sunday Mirror)

Manchester United, Liverpool na Arsenal zote ziko tayari kutuma ofa za kumnunua beki wa pembeni wa Brentford na Scotland Aaron Hickey, 21. (Sunday Mirror)

Mshambuliaji wa Brighton na Jamhuri ya Ireland Evan Ferguson aliamua kuwa kusalia na Seagulls ni bora kwake kuliko kuhamia Manchester United baada ya klabu hiyo kuonyesha nia ya kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18 msimu wa joto. (Sunday Mirror)

Paris St-Germain wanavutiwa na winga wa Real Madrid na Brazil Rodrygo, 22, ili kukabiliana na harakati za wababe hao wa Uhispania za kumnasa mshambuliaji wao wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24. (Football Transfers)

Real pia wana nia ya kumsajili beki wa kushoto wa Canada Alphonso Davies, 22, kutoka Bayern Munich. (Football Transfers)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.