Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amethibitisha kuwa ni kweli beki wao Che Malone Fondo amepata ajali leo Septemba 24 alfajiri akiwa anatoka uwanja wa ndege kupokea ndugu zake waliokuwa wamekuja kumtembelea
Ahmed amesema kuwa tayari mchezaji huyo ameshakamilisha taratibu za hospitali na polisi na sasa ameruhusiwa kwenda nyumbani kupumzika
Hata hivyo amesema beki wao hajaumia kabisa (yupo fiti) katika ajali Ile aliyeumia ni kaka yake ambaye alipata michubuko kidogo.
"Ni kweli Che Malone amepata ajali leo maeneo ya mikocheni na hadi sasa ameshamaliza taratibu zote za hospitali na polisi na amekwenda nyumbani kupumzika," alisema Ahmed