Arsenal wako tayari kuongeza hamu ya kumnunua mshambuliaji wa England Ivan Toney mwezi Januari, huku Brentford wakimpa thamani ya pauni milioni 60 mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Mirror)
Brentford wanafikiria kusajili mshambuliaji mpya Januari hata kama hawatamuuza Toney, huku mchezaji wa kimataifa wa Wolfsburg Mdenmark Jonas Wind, 24, mshambuliaji wa AZ Alkmaar wa Ugiriki Vangelis Pavlidis na mchezaji wa kimataifa wa Brazil wa Santos Marcos Leonardo, 20 wakiwa, kwenye orodha yao fupi. (90min)
Roma wana nia ya kubadilisha mkopo wa mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku kutoka Chelsea kuwa mkataba wa kudumu na wanaweza kumpa mshambuliaji wa Uingereza Tammy Abraham, 25, kwa kubadilishana sehemu. (Calciomercatoweb – In Italy)
Chelsea wameachana kwa siri na Bruno Saltor, ambaye alijiunga na benchi la nyuma la meneja wa zamani Graham Potter na alikuwa kocha wa kikosi cha kwanza chini ya meneja mpya Mauricio Pochettino. (Telegraph – Subscription Required)
Mtendaji mkuu wa Inter Milan Beppe Marotta anasema klabu hiyo hivi karibuni itakutana na mlinzi wa Italia Federico Dimarco, 25, kujadili mkataba mpya. (Radio Anch'Io Sport, via Gazzetta dello Sport) Beki wa Uingereza Fikayo Tomori, 25, alikataa ombi la Paris St-Germain msimu wa joto ili kusalia AC Milan. (Calciomercato – In Italy)
Wachezaji wenza wa Jadon Sancho wa Manchester United wamemtaka winga huyo wa Uingereza, 23, kuomba msamaha na kumaliza mzozo wake na meneja Erik ten Hag. (Mirro)
Chama cha Wanasoka wa Kulipwa (PFA) kimejitolea kusaidia katika jitihada za kuwasaidia Ten Hag na Sancho kumaliza tofauti zao. (Times- Subscription Required)
West Ham wamemaliza nia yao ya kutaka kumsajili winga wa Uingereza Jesse Lingard kwa uhamisho wa bila malipo, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 sasa akiifundisha klabu ya Saudi Pro League Al Ettifaq kwa nia ya kupata kandarasi. (Subscription Required)
Uefa imeshutumiwa kwa kuwasilisha ushahidi "usio wa kweli" kwa uchunguzi wake huru kuhusu machafuko kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa 2022 kati ya Liverpool na Real Madrid mjini Paris. (Guardian)
BBC



