Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Septemba 27 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th September 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Septemba 27 2023

Mkurugenzi wa michezo wa Arsenal Edu amefanya mazungumzo na wakala wa mshambuliaji wa Aston Villa Ollie Watkins kuhusu uhamisho wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza, 27, huku Chelsea pia ikimtaka mchezaji huyo. (Football Transfers)

Aston Villa wamesalia kwenye mazungumzo kuhusu kuongeza mkataba wa Watkins na wanataka mkataba mpya ukamilishwe ifikapo Januari. (90 min)

Arsenal na Chelsea wako tayari kutoa wachezaji pamoja na pesa katika majaribio yao ya kumsajili mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney kutoka Brentford, ambaye kuna uwezekano wa kutaka zaidi ya £75m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (90 min)

Newcastle United wanatazamiwa kuanza mazungumzo na kiungo wa kati wa Brazil Joelinton, 27, na kiungo wa kati wa Uingereza Sean Longstaff, 25, kuhusu kuongeza kandarasi zao, ambazo zote zinatazamiwa kumalizika Juni 2025. (Football Insider)

Barcelona wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Nigeria Wilfred Ndidi, 26, wakati kandarasi yake Leicester City itakapokamilika mwishoni mwa msimu huu. (Sport - kwa Kihispania)

Napoli wanamfuatilia meneja wa zamani wa Paris St-Germain Christophe Galtier kufuatia mwanzo mbaya wa msimu chini ya Rudi Garcia, wakati Marseille pia wanavutiwa na mchezaji huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 57 baada ya kocha wa zamani Marcelino kujiuzulu kwa kushtukiza. (RMC Sport – In French)

Bilionea wa Uingereza Sir Jim Ratcliffe yuko tayari kurekebisha ofa yake ya kuinunua Manchester United ili kufikia makubaliano na wamiliki wa sasa wa Glazers. (Mirror)

Barcelona wamekubali kwa mdomo wa ada ya euro 35m (£30.4m) na Manchester City kubadilisha mkopo wa beki wa pembeni wa Ureno Joao Cancelo kuwa mkataba wa kudumu. (El Chiringuito TV - Spanish)

Mshambulizi wa Slovenia Benjamin Sesko, 20, anasema alizungumza na Manchester United msimu uliopita kabla ya kuondoka Red Bull Salzburg, lakini alihisi kuhamia RB Leipzig kulikuwa bora ili kujiimarisha. (Transfermarkt - Germany)

Reading wamewekewa vikwazo vya kuhama kwa kushindwa kulipa HMRC kwa wakati na wanaweza kukabiliwa na kukatwa pointi zaidi ikiwa watashindwa kulipa mishahara kwa wachezaji na wafanyakazi Ijumaa hii. (Telegraph – Subscription Required)

Chelsea imepewa kibali cha Ligi Kuu ya Uingereza kwa kampuni ya data za michezo ya Infinite Athlete kuwa mdhamini wao wa mbele ya jezi katika mkataba wa thamani ya takriban £40m kwa msimu huu. (Telegraph – Subscription Required)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.