Hersi kuongoza mashabiki wa Yanga Key Day

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th September 2023


Hersi kuongoza mashabiki wa Yanga Key Day

Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amesema atakuwa miongoni mwa Wananchi watakaobeba funguo zao kuhanikiza kwenye mchezo dhidi ya Al Merrikh ambao utapigwa Jumamosi, Septemba 30 katika uwanja wa Azam Complex

Yanga itachuana na Al Merrikh katika mchezo ambao Wananchi wanahitaji kushinda au matokeo yoyote ya sare ili kutinga hatua ya makundi baada ya kusubiri kwa takribani miaka 25

Yanga ina faida ya ushindi wa mabao 2-0 waliopata katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa ugenini nchini Rwanda

Mchezo huo muhimu umebebwa na Stephane Aziz Ki ukipewa jina la Key Day ambapo mashabiki wametakiwa kwenda na funguo zao uwanjani ili kufungua milango ya kwenda makundi huku wale wenye kuvaa 'vinjunga' nao wakipewa nafasi

"Mimi nitakwenda na funguo yangu uwanjani ili kuungana Wanachama na mashabiki  kwenye KI Day . Pale jukwaani tunapokaa viongozi kuna taratibu zake za mavazi, ni ngumu kuvaa bukta, lakini niwahakikishie nitakuwa na funguo yangu mkononi," alisema Hersi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.