Mshambuliaji wa Barcelona na Poland Robert Lewandowski, 35, amesalia kwenye orodha ya wachezaji ambao Saudi Pro League inataka kuwasajili. (Sport - kwa Kihispania)
Arsenal itaendelea kumfuatilia mshambuliaji wa Wolves na Ureno Pedro Neto kwa matumaini ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 katika uhamisho wa Januari. (Mirror)
Arsenal pia inamfuatilia mchezaji wa Sporting Lisbon mwenye umri wa miaka 19 na mlinzi wa Ivory Coast Ousmane Diomande. (Givemesport)
Mkurugenzi wa michezo wa Juventus Cristiano Giuntoli anasema Chelsea ilishindwa kumsajili mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic mwenye umri wa miaka 23 kwa sababu hawakutoa ofa ambayo ilikidhi thamani ya klabu hiyo ya Italia. (La Repubblica, kupitia Goal)
West Ham iliamua kutomsajili mshambuliaji wa Uingereza Jesse Lingard, ambaye ni mchezaji huru baada ya kuondoka Nottingham Forest, kwa sababu mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 hayuko sawa. (Football Insider)
Arsenal, Chelsea na Tottenham Hotspur wameonyesha nia ya kumnunua mshambuliaji wa Feyenoord na Mexico Santiago Gimenez, 22. (Fijaches - kwa Kihispania)
Shirikisho la soka la Saudi Arabia limewatafuta waamuzi wakuu wa Ligi Kuu ya Uingereza akiwemo Michael Oliver kuhusu kuchezesha Ligi ya Saudia. (Telegraph - usajili unahitajika)
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp ana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Uholanzi Donyell Malen, 24, kutoka Borussia Dortmund huku akitafuta mchezaji wa kumsaidia winga wa Misri Mohamed Salah, 31. (Bild, via Express)
Bayern Munich wanajadiliana kuhusu uwezekano wa kumsajili tena beki wa zamani wa Ujerumani Jerome Boateng, 35, ambaye ni mchezaji huru baada ya kuondoka Lyon mwishoni mwa msimu uliopita. (Sky Sports Ujerumani)
Everton wako tayari kumpa mlinzi wa England chini ya umri wa miaka 21, Jarrad Branthwaite, 21, mkataba mpya. (Football Insider)
BBC



