Uongozi Simba wamkingia kifua Robertinho

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd October 2023


Uongozi Simba wamkingia kifua Robertinho

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amehakikishiwa uungwaji mkono na uongozi wa Simba baada ya kufanikiwa kuipeleka Simba hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba zimebainisha kuwa baada ya kikao cha dharura, uongozi umeridhishwa na Robertinho kwa sababu ameendelea kutimiza malengo ya klabu mpaka sasa

Aidha Robertinho amepewa changamoto ya kuhakikisha anaendelea kuimarisha timu hasa kwa maeneo yaliyoonekana kuwa na mapungufu

"Kimsingi hakutakuwa na mabadiliko katika benchi la ufundi. Bodi imeona hakuna sababu ya kumuondoa kocha kwa sababu mpaka sasa timu imefanya vizuri. Kwa nini turekebishe kitu ambacho hakijaharibika?"

"Lakini jambo la msingi ni kuwa benchi la ufundi kwa ujumla limetakiwa kuboresha baadhi ya maeneo ambayo yameonekana kuwa na mapungufu. Bado uongozi una imani na Robertinho kwani mpaka sasa amefanikisha malengo," alieleza mtoa taarifa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.