Yanga - Local - Transfer

Kocha Yanga adokeza maboresho ya kikosi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Oct 2023
Kocha Yanga adokeza maboresho ya kikosi

Kabla ya kuanza kwa mechi za hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika (CAF CL), dirisha la usajili la CAF linatarajiwa kufunguliwa kwa timu ambazo katika awamu ya kwanza ya usajili hazikutimiza wachezaji 40

Hii inaweza kuwa nafasi nyingine kwa Yanga kuimarisha kikosi zaidi kwa ajili ya mikiki mikiki ya kuanzia hatua ya makundi kwani katika awamu ya kwanza ya usajili Yanga iliandikisha wachezaji 29

Katika moja ya mahojiano yake baada ya mchezo dhidi ya Al Merrikh ambao Yanga ilikata tiketi ya kutinga makundi, Mkufunzi wa Yanga Miguel Gamondi alidokeza uhitaji wa maboresho kwenye maeneo machache

"Tunakwenda kushindana kwenye hatua ya makundi. Ili tuwe washindani bora zaidi ni wazi tutahitaji maboresho katika maeneo machache, hilo liko ndani ya mipango ya uongozi lakini kama kocha, wakati wote unahitaji zaidi"

"Pasipo na shaka, tunahitaji maboresho kidogo ili tuwe washindani bora zaidi dhidi ya timu kubwa," alisema Gamondi

Eneo ambalo Gamondi alilenga ni wazi ni katika safu ya ushambuliaji ambapo bado usajili wa Mghana Hafiz Konkoni 'haujawaka'

Katika mechi za karibuni Gamondi amewatumia zaidi Clement Mzize na Kennedy Musonda wakati Konkoni akipata dakika chache kwenye baadhi ya mechi

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
3h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
7h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
8h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
9h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
9h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
10h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
10h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’