Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Oktoba 07 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th October 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Oktoba 07 2023

Manchester City wanafahamu kuwa mshambuliaji wa Norway Erling Haaland ana nia ya kuichezea Real Madrid lakini wanataka kuanza mazungumzo kuhusu kuongeza mkataba wake, huku mkataba wa sasa wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ukiendelea hadi Juni 2027. (ESPN)

Meneja wa zamani wa Swansea na Leeds United, Garry Monk ni jina linalohusishwa na kuchukua nafasi ya Andrea Pirlo huko Sampdoria. (SampNews24, via Sun)

Chelsea wanasubiri kuona iwapo mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen atasaini mkataba mpya na Napoli, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 na mwakilishi wake bado wakiwa bado hawajafanya uamuzi wa kusalia katika klabu hiyo ya Italia au la. (90 Min)

Brentford wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Southampton Carlos Alcaraz mwezi Januari, huku The Bees wakiwa wameshindwa na kumsajili Muargentina huyo alipojiunga na klabu hiyo ya pwani ya kusini mwezi Januari - ingawa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 alitia saini mkataba mpya Saints siku ya Ijumaa. ((Standard)

Barcelona wanafikiria kumrejesha mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi, 36, katika timu yake ya utotoni kwa mkopo mwezi Januari ikiwa Inter Miami itashindwa kufikia hatua ya mtoano ya MLS. (Sport, via Mail)

Timu ya League ya Kwanza Burton Albion imechapisha chapisho la siri ikiukejeli uwezekano wa kurejea katika soka kwa mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Tottenham na England Peter Crouch , 38 . (Mail)

Mshindi wa Kombe la Dunia la Ujerumani Jerome Boateng, 35, hana klabu baada ya kushindwa kupata kandarasi na timu yake ya zamani Bayern Munich. (Sun)

Winga wa zamani wa Tottenham, Crystal Palace na England Andros Townsend, 32, yuko kwenye majaribio Luton Town na anakaribia kusaini kandarasi na wachezaji wapya wa Premier League. (Express)

Mlinzi wa Crystal Palace Tyrick Mitchell, 24, anaangalia uwezekano wa kubadili kutoka Uingereza na kuelekea Jamaica. (Mail)

Bradford City wamewalenga Steve Thompson na Neil Redfearn katika kutafuta meneja mpya kuchukua nafasi ya Mark Hughes. (Star)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.