Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kimeingia kambini kujiandaa na mchezo wa Kimataaifa wa kirafiki dhidi ya Sudan ambao utapigwa Oktoba 15 huko Saudi Arabia
Wachezaji Baraka Majorogo kutoka Chippa United ya Afrika Kusini na George Mpole kutoka FC Lupopo (DR Congo) ni miongoni mwa wachezaji wapya waliojumuishwa katika kikosi hicho
Kocha Mkuu wa Stars Adel Amrouche amewaita wachezaji walewale aliowatumia kwenye mchezo dhidi ya Aleria mwezi uliopita







