Mkude arejea kikosini Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th October 2023


Mkude arejea kikosini Yanga

Kiungo wa Yanga Jonas Mkude jana alirejea kwenye mazoezi ya mabingwa hao watetezi ligi kuu ya NBC baada ya kukosekana kwa wiki kadhaa

Imeelezwa Mkude na mlinda lango Metacha Mnata walisimamishwa na uongozi wa Yanga kutokana na matatizo ya utovu wa nidhamu

Jana Yanga ilianza maandalizi ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Oktoba 25 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Metacha naye amemaliza adhabu, amejumuishwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania kinachojiandaa na mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sudan ambao utapigwa Saudi Arabia Oktoba 15

Mkude amekuwa akikumbwa na matukio ya kinidhamu mara kwa mara tangu wakati akiitumikia Simba


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.