Kiungo wa Yanga Jonas Mkude jana alirejea kwenye mazoezi ya mabingwa hao watetezi ligi kuu ya NBC baada ya kukosekana kwa wiki kadhaa
Imeelezwa Mkude na mlinda lango Metacha Mnata walisimamishwa na uongozi wa Yanga kutokana na matatizo ya utovu wa nidhamu
Jana Yanga ilianza maandalizi ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Oktoba 25 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Metacha naye amemaliza adhabu, amejumuishwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania kinachojiandaa na mchezo wa Kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sudan ambao utapigwa Saudi Arabia Oktoba 15
Mkude amekuwa akikumbwa na matukio ya kinidhamu mara kwa mara tangu wakati akiitumikia Simba



