Shirikisho la Soka Afrika (CAF ) usiku wa jana lilipanga Makundi sita yenye Timu nne zitakazoshiriki michuano ya AFCON 2023 nchini Ivory Coast kuanzia January 13 2024
Tanzania imepangwa Kundi F sambamba na timu namba moja kwa ubora barani Afrika, Morocco washiriki wa nusu fainali ya kombe la Dunia 2022. Katika kundi hilo pia zimo Congo DR na Zambia
Mechi zao zitachezwa katika Mji wa San-Pedro nchini Ivory Coast ambapo ni umbali wa Kilometa 337 kwa gari kutokea mji Mkuu wa nchi hiyo Abidjan




