Tanzania uso kwa uso na Morocco Afcon 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th October 2023


Tanzania uso kwa uso na Morocco Afcon 2023

Shirikisho la Soka Afrika (CAF ) usiku wa jana lilipanga Makundi sita yenye Timu nne zitakazoshiriki michuano ya AFCON 2023 nchini Ivory Coast kuanzia January 13 2024

Tanzania imepangwa Kundi F sambamba na timu namba moja kwa ubora barani Afrika, Morocco washiriki wa nusu fainali ya kombe la Dunia 2022. Katika kundi hilo pia zimo Congo DR na Zambia

Mechi zao zitachezwa katika Mji wa San-Pedro nchini Ivory Coast ambapo ni umbali wa Kilometa 337 kwa gari kutokea mji Mkuu wa nchi hiyo Abidjan


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.