Katika mazoezi ya Yanga yanayoendelea Avic Town kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc ambao umesogezwa nyuma kutoka Oktoba 25 mpaka Oktoba 22, kuna nyota mpya ameonekana
Ni mlinda lango Ndizeye Aime aliyeonekana katika viunga vya Avic Town wiki hii akijifua kwenye kikosi cha kocha Miguel Gamondi
Aime mwenye umri wa miaka 21, msimu uliopita aliitumikia Aigle Noir ya Burundi
Hata hivyo taarifa za uhakika ni kuwa mlinda lango huyo hajasajiliwa bali amepewa nafasi ya kufanya mazoezi na timu wakati huu wachezaji wengi wakiwa wameondoka kutimiza majukumu ya timu za Taifa
Yanga inawakosa wachezaji 10 ambao wanatekeleza majukumu ya timu za Taifa kwenye mechi za Kimataifa za kirafiki zilizo kwenye kalenda ya FIFA
Lakini hii inaweza kuwa fursa nzuri kwake kama ataweza kumshawishi Gamondi anaweza kumuweka kwenye orodha ya nyota wapya atakaowasajili



