Kipa Aigle Noir afanya majaribio Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th October 2023


Kipa Aigle Noir afanya majaribio Yanga

Katika mazoezi ya Yanga yanayoendelea Avic Town kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc ambao umesogezwa nyuma kutoka Oktoba 25 mpaka Oktoba 22, kuna nyota mpya ameonekana

Ni mlinda lango Ndizeye Aime aliyeonekana katika viunga vya Avic Town wiki hii akijifua kwenye kikosi cha kocha Miguel Gamondi

Aime mwenye umri wa miaka 21, msimu uliopita aliitumikia Aigle Noir ya Burundi

Hata hivyo taarifa za uhakika ni kuwa mlinda lango huyo hajasajiliwa bali amepewa nafasi ya kufanya mazoezi na timu wakati huu wachezaji wengi wakiwa wameondoka kutimiza majukumu ya timu za Taifa

Yanga inawakosa wachezaji 10 ambao wanatekeleza majukumu ya timu za Taifa kwenye mechi za Kimataifa za kirafiki zilizo kwenye kalenda ya FIFA

Lakini hii inaweza kuwa fursa nzuri kwake kama ataweza kumshawishi Gamondi anaweza kumuweka kwenye orodha ya nyota wapya atakaowasajili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.