Kocha wa Roma Jose Mourinho anatarajiwa kuondoka katika klabu hiyo ya Italia mkataba wake utakapokalizika mwishoni mwa msimu huu, hakuna mazungumzo yoyote kuhusu yaliyofanywa kuhusu kuongezwa kwa mkataba wake. (Sky Sports Italia, kupitia Football Italia)
Kocha wa zamani wa Juventus, Chelsea na Tottenham Antonio Conte anasema siku moja angevutiwa kuinoa Roma au Napoli, na kwamba alikataa timu ya taifa ya Saudi Arabia. (Il Corriere della Sera, kupitia Football Italia)
Juventus wanaendelea kumfuatilia kiungo wa kati wa Denmark Pierre-Emile Hojberg, 28
Manchester United wanapania kumnunua beki wa Crystal Palace na Uingereza Marc Guehi, 23, ambaye amekuwa akihusishwa na llabu kadhaa za Ligi ya Premia. (Football Insider)
Aston Villa wanafikiria kumpa Leon Bailey kandarasi mpya, huku mkataba wa sasa wa winga huyo wa Jamaica mwenye umri wa miaka 26 ukikamilika Juni 2025. (Football Insider)
Arsenal wana uhakika wa kukubaliana mkataba mpya na beki wa Uingereza Ben White, 26, ambaye ana furaha katika klabu hiyo. (Fabrizio Romano)
Everton wanavutiwa na winga wa Corinthians wa Brazil Wesley Gassova, 18 - lakini watakabiliwa na ushindani. (Teamtalk)
Beki wa kati wa Ujerumani Malick Thiaw, 22, anataka kusalia AC Milan licha ya kutakiwa na Real Madrid na West Ham. (Calcio Mercato)
Borussia Monchengladbach wataanzisha kipengele cha kuongeza mkataba wa kiungo Mfaransa Manu Kone mwenye umri wa miaka 21 kwa mwaka mmoja ili uendelee hadi 2026. (Rheinische Post, via Get German Football News)
Kiungo wa kati wa Ubelgiji Romeo Lavia, 19, ambaye bado hajacheza mechi yake ya kwanza Chelsea tangu ajiunge nayo kutoka Southampton msimu wa joto, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja hadi mwisho wa Novemba kutokana na jeraha la kifundo cha mguu alilolipata akiwa mazoezini. (Mail)
BBC