Yanga - Azam - Local

Je Yanga itaendeleza ubabe dhidi ya Azam Fc Jumapili?

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Oct 2023
Je Yanga itaendeleza ubabe dhidi ya Azam Fc Jumapili?

Jumapili ya wiki hii nyasi za uwanja wa Azam Complex zitawaka moto pale mabingwa wa ligi kuu ya NBC Yanga watakaposhuka uwanjani kuikabili Azam Fc katika mchezo wa ligi

Ni mchezo ambao Yanga itakuwa mwenyeji, Yanga ilichagua kucheza mechi zake za nyumbani hapo Azam Complex baada ya uwanja wa Benjamin Mkapa kufungwa kwa ajili ya ukarabati

Awamu ya kwanza ya ukarabati uwanja wa Mkapa imekamilika lakini uwanja huo utafunguliwa kwa ajili ya mechi za AFL na mchezo dhidi ya Simba utakaopigwa Novemba 05 ambapo baada ya mchezo huo uwanja utafungwa tena kwa ajili ya awamu ya pili ya ukarabati

Habari njema kwa Yanga ni kuwa wachezaji wameuzoea uwanja wa Azam Complex kwani mechi zote tatu za nyumbani kwenye ligi kuu na mechi nyingine tatu kwenye ligi ya mabingwa zote zilipigwa Azam Complex

Yanga ina rekodi ya aina yake katika mechi ilizocheza dimba la Azam Complex, mara ya mwisho kupoteza mchezo kwenye uwanja huo ilikuwa Januari 2020

Aidha Wananchi hawajapoteza mchezo wowote dhidi ya Azam Fc katika mechi sita zilizopita, ushindi ni mechi tano na sare ni mechi moja

Sare pekee waliyopata Azam Fc ni msimu uliopita kwenye ligi kuu ya NBC. Mara ya mwisho kwa Azam Fc kupata ushindi dhidi ya Yanga ni April 25 2021 ukiwa ni mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Kabla ya kuanza msimu huu, Yanga na Azam Fc zilikutana kwenye Ngao ya Jamii mkoani Tanga Yanga ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’