Maboresho makubwa yamefanyika uwanja wa Mkapa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th October 2023


Maboresho makubwa yamefanyika uwanja wa Mkapa

Awamu ya kwanza ya maboresho ya uwanja wa Benjamin Mkapa iko mbioni kukamilika kuelekea ufunguzi wa michuano ya African Football League utakaofanyika siku ya Ijumaa, Oktoba 20

Simba wenyeji wa michuano hiyo wataumana na Al Ahly katika mchezo ambao unatarajiwa kufuatiliwa dunia nzima

Wakati zoezi la kubadilisha viti likitarajiwa kufanyiwa baada ya AFL, kuna maboresho makubwa yamefanyika uwanjani kuanzia eneo la kuchezea 'pitch' na mabenchi ya ufundi

Leo zoezi la kufunga viti vipya kwenye mabenchi ya ufundi lilifanyika. Eneo la kuzunguuka uwanja pia yamefungwa mabango ya kidigitali ambayo yataanza kutumika rasmi siku ya Ijumaa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.