Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Oktoba 19 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th October 2023


Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Oktoba 19 2023

Liverpool wameungana na Chelsea na Arsenal katika kinyang'anyiro cha kumsaka mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24, ambaye anakadiriwa kuwa pauni milioni 95. (Sun)

Mshambulizi wa Argentina Lionel Messi, 36, amepuuza tetesi kwamba ataondoka Inter Miami kwa mkopo kwenda kuchezea klabu nyingine mara tu msimu wa MLS utakapomalizika. (ESPN)

Inter Miami wanatarajia kumleta mshambuliaji wa Uruguay na Gremio Luis Suarez, 36, kwenye klabu ili kuungana na mchezaji mwenza wa zamani wa Barcelona Messi. (Mirror)

Mlinzi wa Chelsea Mbrazil Thiago Silva, 39, amedokeza kurejea Fluminense mwaka ujao, huku mkataba wake na The Blues ukitarajiwa kukamilika msimu huu wa joto. (Sun)

Bayern Munich wanapania kumnunua mlinzi wa zamani wa Arsenal Mgiriki Sokratis Papastathopoulos, 35, huku wakijaribu kupunguza athari ya majeraha yanayowakabili wachezaji. (Mirror)

Borussia Monchengladbach wameanzisha chaguo la kuongeza kandarasi ya kiungo wa kati wa Ufaransa Manu Kone huku Liverpool, Juventus na Bayern Munich wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22. (90 min)

Newcastle wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Bayer Leverkusen na Nigeria Victor Boniface, 22. (Sun)

Bayern Munich wana uhakika wa kumsainisha kiungo wa kati wa Ujerumani Jamal Musiala kwenye mkataba mpya huku Liverpool na Manchester City zikiwa na nia ya kumsajili ingawa kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 inaendelea hadi 2026. (90 min)

Nyota wa zamani wa West Ham Muitaliano Paolo di Canio, 55, amefichua kuwa alikataa nafasi ya kujiunga na safu ya ukufunzi ya Roberto Mancini katika timu ya taifa ya Saudi Arabia. (La Stampa, via Sun)

Rangers wamemwendea mkuu wa uajiri wa Brighton Sam Jewell, ambaye yuko nyuma ya wachezaji wakubwa waliosajiliwa na Seagulls. (Star)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.