Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Oktoba 21 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st October 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi Oktoba 21 2023

Rais wa Napoli Aurelio De Laurentiis amesema mshambuliaji Victor Osimhen, 24, atauzwa huku Arsenal , Chelsea na Liverpool zikiwa na nia ya kutaka kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Nigeria. (Metro)

Liverpool inamwona Osimhen kama mbadala wa mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah, 31, ambaye amekuwa akihusishwa pakubwa na kuhamia Saudi Pro League. ( Mirror)

Real Madrid wanatazamia uhamisho wa pauni milioni 35 kumnunua beki wa kushoto wa Bayern Munich na Canada Alphonso Davies, 22, atakapoingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake na mabingwa wa Ujerumani mwaka 2024. (Bild - in German)

Newcastle wanakabiliwa na vita vya kuwashawishi Manchester City kumtoa kwa mkopo kiungo wa kati Kalvin Phillips mwenye umri wa miaka 27 mwezi Januari, huku Bayern Munich wakiwa tayari kuchukua hatua ya kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza. (Sun)

Juventus pia wanavutiwa na Phillips pamoja na kiungo wa kati wa Atletico Madrid na Argentina Rodrigo De Paul, 29, na kiungo wa kati wa Tottenham na Denmark Pierre-Emile Hojbjerg, 28. (Gazzetta dello Sport - in Italian)

Real Madrid wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Argentina na Manchester City Julian Alvarez, 23, ili kuimarisha kikosi cha Carlo Ancelotti katika La Liga. (Sebastián Srur, via Mail)

Tottenham na West Ham zote zinamfuatilia mlinzi wa Chelsea Trevoh Chalobah, 24, huku beki huyo wa kati wa zamani wa England chini ya umri wa miaka 21 pia akivutia Ujerumani na Italia. (Teamtalk)

Chelsea wako tayari kumruhusu mlinzi wa Brazil Thiago Silva, 39, kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu mkataba wake utakapokamilika huku wakipania kuwakuza wachezaji wao wachanga. (Football Insider)

Arsenal ina orodha fupi ya wachezaji wanne wanaolengwa katika dirisha la usajili la Januari licha ya kuwa na bajeti ndogo tu, huku mshambuliaji wa Brentford Muingereza Ivan Toney, 27, akiwa wa kwanza kulengwa. (Mirror)

Sporting Lisbon haitamruhusu mshambuliaji wa Uswidi Viktor Gyokeres, 25, kuondoka isipokuwa mtu afikie kipengee chake cha kumuachilia cha euro milioni 100, huku klabu kadhaa za Premier League na Serie A zikiwa na nia ya kumnunua mshambuliaji huyo. (Record - in Portuguese)

Liverpool bado wana uhakika wa kumsajili kiungo wa kati wa Fluminense na Brazil Andre, 22, licha ya Premier League Arsenal kuonyesha nia. (Football Insider)

Manchester United na Newcastle United ni miongoni mwa vilabu vinavyofikiria kumnunua kiungo wa kati wa Valencia na Uhispania Javi Guerra Januari 20. (Fichajes - in Spanish)

Bosi wa zamani wa Marekani Bruce Arena, 72, anagombea kuchukua nafasi ya Wayne Rooney kama meneja wa klabu ya Ligi Kuu ya Soka ya DC United . (Athletic - subscription required)

Mkurugenzi wa michezo wa Barcelona Deco anasema fedha zilimzuia mshambuliaji wa Brazil Neymar, 31, kurejea katika klabu hiyo ya La Liga msimu wa joto kabla ya kujiunga na klabu ya Al-Hilal ya Saudia kutoka Paris St-Germain. (90min)

Manchester City wanaweza kushindana na Barcelona na Real Madrid katika kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa kulia wa Girona Arnau Martinez, 20 , ambaye ameiwakilisha timu ya Uhispania ya Under-21. (90min)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.