Wakati Ligi Kuu ya NBC ikiingia mzunguuko wa sita, tayari makocha watano wamepoteza ajira zao kutokana na matokeo mabaya
Jana Kocha wa Namungo Fc Cedric Kaze alitangaza kuachia ngazi kufuatia mfululizo wa matokeo mabaya
Katika mechi sita ambazo Kaze aliiongoza Namungo Fc, aliambulia sare tatu tu huku timu hiyo ikipoteza mechi tatu
Kipigo cha mwisho kilikuwa nyumbani Ruangwa dhidi ya Singida BS, Namungo Fc wakichapwa mabao 3-2
Makocha wengine ambao wamepoteza nafasi zao kwenye ligi kuu ni Zuberi Katwila (Ihefu Fc), Habibu Kondo (Mtibwa Sugar), Ernst Middendorp na Hans van Pluijm wote kutoka Singida BS



