Makocha watano wapoteza ajira NBC PL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd October 2023


Makocha watano wapoteza ajira NBC PL

Wakati Ligi Kuu ya NBC ikiingia mzunguuko wa sita, tayari makocha watano wamepoteza ajira zao kutokana na matokeo mabaya

Jana Kocha wa Namungo Fc Cedric Kaze alitangaza kuachia ngazi kufuatia mfululizo wa matokeo mabaya

Katika mechi sita ambazo Kaze aliiongoza Namungo Fc, aliambulia sare tatu tu huku timu hiyo ikipoteza mechi tatu

Kipigo cha mwisho kilikuwa nyumbani Ruangwa dhidi ya Singida BS, Namungo Fc wakichapwa mabao 3-2

Makocha wengine ambao wamepoteza nafasi zao kwenye ligi kuu ni Zuberi Katwila (Ihefu Fc), Habibu Kondo (Mtibwa Sugar), Ernst Middendorp na Hans van Pluijm wote kutoka Singida BS


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.