Manchester City wana imani fowadi wa Argentina Julian Alvarez, 23, atasalia katika klabu hiyo licha ya kuripotiwa kuvutia hamu Barcelona na Real Madrid. (Football Insider)
Arsenal bado ina nia ya kujaribu kumsajili kiungo wa kati wa Brazil Douglas Luiz, 25, kutoka Aston Villa baada ya ofa kadhaa kukataliwa. (90 min)
Everton wana wasiwasi na taarifa ya Al-Ettifaq kutaka kumnunua mshambuliaji wa Uingereza Dominic Calvert-Lewin, 26, huku hali ya sintofahamu ya kumchukua ikiendelea. (Football Insider)
Manchester United wako tayari kwa ofa yoyote ya Januari kwa ajili ya kumuuza Jadon Sancho, 23, huku kazi ya winga huyo wa kimataifa wa Uingereza katika klabu ya United ikiwa imekwisha kwa "90% zaidi". (Fabrizio Romano, kupitia Sun)
Winga wa Fiorentina na Argentina Nicolas Gonzalez, 25, anavutia klabu kadhaa za Premier League baada ya kuanza vyema kwa kampeni ya sasa. (La Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)
West Ham inamfuatilia mshambuliaji wa AZ Alkmaar na Ugiriki Vangelis Pavlidis, 24, huku wakitafuta kuimarisha safu yao ya ushambuliaji. (90 min)
Manchester City wako tayari na kufikiria kuhama kwa kiungo wao wa kati wa Uingereza Kalvin Phillips, 27, mwezi Januari, huku mchezaji huyo akiwekwa benchi na meneja Pep Guardiola. (Fabrizio Romano)
Mlinda mlango wa Burnley na Kosovo Arijanet Muric, 24, anavutia klabu kadhaa vikiwemo Union Berlin na Sevilla. (Sky Sport Deutschland)
Sevilla pia wanafuatilia mustakabali wa kiungo wa kati wa Manchester United na Tunisia Hannibal Mejbri, 20. (Offside)
Tottenham ni miongoni mwa timu zinazomfuatilia beki wa kati wa Club America na Uruguay Sebastian Caceres, 24. (Football Insider)
Inter Milan, klabu ya zamani ya AC Milan na Juventus wote wanavutiwa na beki wa kati wa Lille Tiago Djalo, 23, huku mkataba wa mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Ureno chini ya miaka 21 ukikamilika msimu wa joto. (La Gazzetta dello Sport – In Italy)
Ajax huenda ikashindwa na mbinu yoyote ya kumnasa meneja msaidizi wa Manchester United Mitchell van der Gaag kurejea klabuni hapo kuchukua nafasi ya kocha Maurice Steijn, ambaye amewaacha wababe hao wa Uholanzi kufuatia mwanzo mbaya wa msimu. (The Mail)
Mkufunzi wa Bournemouth Andoni Iraola anakabiliwa na mazungumzo wiki hii na anaweza kuwa meneja wa kwanza wa Premier League kutimuliwa msimu huu. (Sun)
BBC