Al Ahly vs Simba kinapigwa Misri leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th October 2023


Al Ahly vs Simba kinapigwa Misri leo

Kikosi cha Simba kiko nchini Misri ambapo leo Wekundu hao wa Msimbazi wanakabiliwa na mchezo muhimu wa kuwania tiketi ya kutinga nusu fainali African Football League dhidi ya Al Ahly

Mchezo huo utapigwa saa 11 jioni katika uwanja wa Kimataifa wa Cairo

Hii ni mechi ya kuamua hatma ya tmu inayokwenda nusu fainali baada ya mchezo wa mkondo wa kwanza ulopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa kumalizika kwa matokeo ya sare ya mabao 2-2

Haijawahi kuwa rahisi kwa timu yoyote kupata ushindi dhidi ya Al Ahly wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani lakini timu kubwa zina tabia ya kupata matokeo mazuri katika uwanja wowote

Kwa hatua ambayo Simba imefika, hakuna hofu ya kucheza na yeyote iwe nyumbani au ugenini

Msimu uliopita kila mmoja anakumbuka kiwango bora walichoonyesha Simba kule Morocco kwenye robo fainali ya ligi ya mabingwa dhidi ya Wydad Athletic, ilikosekana bahati tu kwenye changamoto ya mikwaju ya penati

Ni mechi ambayo Simba inahitaji matokeo ya aina mbili tu, ushindi au sare ya kuanzia 3-3 ili kutinga nusu fainali. Kama timu hizo zitatoka sare ya mabao 2-2, changamoto ya penati itatumika kumpaka mshindi. Bado CAF wameweka msimamo katika bao la ugenini katika mashindano yao


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.