Wauza jezi feki wamtishia Afisa Habari Yanga

Joel JJ By Joel JJ • 26th October 2023


Wauza jezi feki wamtishia Afisa Habari Yanga

Jana Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe alikumbana na wakati mgumu baada ya kutaka kushambuliwa na wanaodaiwa kuwa wasambazaji wa jezi feki za klabu ya Yanga na Simba

Tukio hilo liilotokea Temeke katika godown lililobainika kuhifadhi shehena ya jezi hizo feki zenye thamani ya Tsh Bilioni 10

Kamwe aliambatana na Waandishi wa habari kuwafichua wezi hao huku akiitaka Serikali iingilie kati kwani watu hao sio tu wanayima mapato klabu pia hawalipi ushuru wa Serikali

Wakati Ally alipofika eneo la tukio mlinzi wa eneo hilo alianza kuleta vitisha vya kutaka kumpiga kabla ya baadhi ya watu kumzuia

Tukio hilo lilirekodiwa 'mbashara' na kuwafanya watuhumiwa hao ambao walikuwa kwenye jitihada za kuhamisha shehena hiyo kushindwa

Ni wazi vita hii ni kubwa na inahitaji sapoti kubwa ya vyombo vya Serikali likiwemo Jeshi la Polisi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.