Jumamosi, Oktoba 28 2023 Simba itashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili Ihefu Fc katika mchezo wa ligi kuu ya NBC
Huu utakuwa mchezo wa kwanza kwa Simba kwenye ligi baada ya ushiriki wake katika michuano ya African Football League (AFL) juzi wakitolewa na Al Ahly kikanuni baada ya sare ya mabao 3-3 katika mechi zote mbili
Kuelekea mchezo huo, Simba imetangaza viingilio ambao VIP A ni Tsh 15,000/-, VIP B ni Tsh 10,000/- na Mzunguuko ni Tsh 5,000/-
Mchezo utapigwa kuanzia saa 1 usiku, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba Ahmed Ally akiwataka Wanasimba kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo huo ili kuonyesha wako pamoja na wachezaji wao licha ya kile kilichotokea kwenye AFL
