Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa Oktoba 27 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th October 2023


Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa Oktoba 27 2023

Maafisa wa ligi ya Pro League nchini Saudia sasa wanamtaka kiungo wa kati wa Manchester City na Ubelgiji Kevin de Bruyne, 32, kujiunga na ligi hiyo huko Mashariki ya Kati mwaka wa 2024(Football Insider)

Newcastle wanalenga kumnunua kiungo wa kati wa Al-Hilal na Ureno Ruben Neves, 26, baada ya Sandro Tonali kupigwa marufuku ya miezi 10 kwa kukiuka kamari. (Sun)

Chelsea wameonyesha nia ya kutaka kumsajili kiungo wa kati wa Uhispania Gavi, 19, ambaye Barcelona wanaweza kumuuza kwa £87m ili kupunguza matatizo yao ya kifedha. (Sport kupitia Express)

Uhamisho wa mkopo kwenda Saudi Arabia ndio njia inayowezekana zaidi ya winga wa Manchester United na Uingereza Jadon Sancho 23 kuondoka katika klabu hiyo ingawa Chelsea wanaweza kuwa chaguo huku Borussia Dortmund wakimpuuza. (Athelet)

Arsenal wametanguliza nia ya kumsaini nyota wa Real Madrid na Ufaransa Aurelien Tchouameni, 23, msimu ujao huku wakimtafuta kiungo wa kucheza pamoja na Declan Rice wa Uingereza. (Football Transfers)

The Gunners pia wamemtambua Martin Zubimendi wa Real Sociedad kama mchezaji wanayemlenga , ingawa kiungo huyo wa kati wa Uhispania mwenye umri wa miaka 24 pia anaivutia Manchester United. (Football Transfers)

Liverpool wamepewa nafasi kubwa ya kumsajili beki wa kati wa Ureno Goncalo Inacio, 22, kutoka Sporting Lisbon. (Bild – Deustch)

Beki wa Fulham Tosin Adarabioyo yuko tayari kuzungumzia mkataba mpya wa muda mrefu baada ya kuona kocha wa Cottagers Marco Silva akisaini mkataba mpya. Ofa ya Monaco kutaka kumnunua Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 26 ilikataliwa msimu uliopita, huku Tottenham pia wakivutiwa. (Standard)

Newcastle United ndio klabu ya hivi punde zaidi ya Ligi ya Premia kufikiria kumnunua Federico Dimarco wa Inter Milan, huku mlinzi huyo wa Italia mwenye umri wa miaka 25 akivutia Chelsea na Manchester United. (Fichajes – In Spanish)

Newcastle wanachunguza uwezekano wa kupunguza mshahara wa Sandro Tonali baada ya kiungo huyo wa kati wa Italia, 23, kupigwa marufuku miezi 10 kwa kukiuka kamari. (Telegraph) Ingechukua ofa ya angalau £80m kwa Manchester City kufikiria kumuuza fowadi wa Argentina Julian Alvarez, 23. (Football Insider)

Mchezaji anayelengwa na West Ham na Brentford Serhou Guirassy, 23, atapatikana kwa takriban £15.2m mwezi Januari kwa sababu ya kipengele cha kutolewa katika mkataba wa mshambuliaji huyo wa Guinea na Stuttgart. (90min)

Sheffield United inaweza kumfuta kazi meneja Paul Heckingbottom, 46, ikiwa timu yake itashindwa na Arsenal siku ya Jumamosi, na kumfungulia njia mkufunzi wa zamani wa Blades Chris Wilder, 53, ambaye kibarua chake cha mwisho kilikuwa Watford msimu uliopita. (Mail)

Kiungo wa kati wa Mali Abdoulaye Doucoure, 30, anatazamiwa kusaini mkataba mpya Everton hadi 2025, na chaguo lake hadi 2026. (Fabrizio Romano)

Chelsea wanafuatilia kwa karibu maendeleo ya mlinzi wa kati wa Lille Mfaransa Leny Yoro, 17. (90min)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.