Serikali yatoa siku saba sakata la jezi feki

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th October 2023


Serikali yatoa siku saba sakata la jezi feki

Waziri wa Viwanda, Uwekezaji na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji amewataka Wafanyabiashara kuacha kukimbilia Polisi pale wanapopata changamoto ya kibiashara badala yake waende Tume ya Ushindani (FCC)

Dkt Ashatu aliyasema hayo jana baada ya kutembelea na kukagua ghala lililobainika kuhifadhi jezi bandia za timu za Azam FC, Yanga SC, Simba FC na timu ya Taifa Tanzania

Waziri huyo amesema Taasisi ya kwanza inayotakiwa kupelekewa malalamiko ni FCC kwa sababu ndiyo yenye mamlaka ya kulinda watumiaji kubaini bidhaa ni bandia au sio bandia, lakini pia kulinda ushindani wenye ufanisi katika biashara

Aidha Dkt Ashatu ametoa siku saba kwa Mkurugenzi wa tume hiyo Wiliam Erio kujiridhisha na kujua idadi halisi ya T-shirt na jezi zote zilipo ili kuhitimisha jambo hili na kushughulika na watuhumiwa wanaomiliki mzigo huo unaokadiriwa kuwa na thamani ya Tsh Bilioni 10


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.