Yanga yaichapa Singida BS 2-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th October 2023


Yanga yaichapa Singida BS 2-0

Mabingwa watetezi ligi kuu ya NBC Yanga wameendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida BS katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Yanga ilifunga mabao yake kupitia kiungo mshambuliaji Maxi Nzengeli aliyefikisha mabao matano kwenye ligi

Ulikuwa mchezo wa upande mmoja kwa muda mwingi Singida BS wakicheza kwa kujihami zaidi kabla ya kuzinduka kwenye dakika 20 za mwisho kwenye kipindi cha pili

Ni ushindi ambao unaifanya Yanga iendelee kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 18

Katika mchezo uliopigwa mapema, KMC ilivutwa shati na Prisons ikilazimishwa sare ya bao 1-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.