Mabingwa watetezi ligi kuu ya NBC Yanga wameendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida BS katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Yanga ilifunga mabao yake kupitia kiungo mshambuliaji Maxi Nzengeli aliyefikisha mabao matano kwenye ligi
Ulikuwa mchezo wa upande mmoja kwa muda mwingi Singida BS wakicheza kwa kujihami zaidi kabla ya kuzinduka kwenye dakika 20 za mwisho kwenye kipindi cha pili
Ni ushindi ambao unaifanya Yanga iendelee kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 18
Katika mchezo uliopigwa mapema, KMC ilivutwa shati na Prisons ikilazimishwa sare ya bao 1-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru



