Mwishoni mwa msimu uliopita aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele alitoa kauli ambayo iliwaibua mabosi wa Azam Fc juu ya mwenendo wa timu hiyo
Mayele ambaye kwa sasa anaitumikia Pyramids Fc ya Misri alisema Azam Fc wanapaswa kubadilika kwa sababu wanacheza mechi kwa kukamia
"Azam Fc ni timu yenye wachezaji wazuri lakini wanakamia mechi. Wanapokutana na Simba na Yanga utawaona wachezaji wao wazuri lakini wakikutana na timu kama Namungo au nyingine huwaoni wachezaji hao," alisema Mayele
Ni kauli ambayo inaendelea kudhihiri baada ya Azam Fc jana kukubali kichapo cha mabao 3-1 dhidi ya Namungo Fc katika uwanja wao wa nyumbani, Azam Complex
Ulikuwa mchezo wa pili mfululizo ambao Azam Fc wanapoteza kwani mchezo uliopita walifungwa na Yanga mabao 3-2
Azam Fc walikuwa bora sana kwenye mchezo dhidi ya Yanga wakitoa upinzani mkali kwa mabingwa hao watetezi lakini jana walionekana kuzidiwa na Namungo
Kipigo hicho kinaweza kumuweka matatani kocha wa timu Youssouf Dabo



