Kauli ya Mayele inawatesa Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th October 2023


Kauli ya Mayele inawatesa Azam Fc

Mwishoni mwa msimu uliopita aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele alitoa kauli ambayo iliwaibua mabosi wa Azam Fc juu ya mwenendo wa timu hiyo

Mayele ambaye kwa sasa anaitumikia Pyramids Fc ya Misri alisema Azam Fc wanapaswa kubadilika kwa sababu wanacheza mechi kwa kukamia

"Azam Fc ni timu yenye wachezaji wazuri lakini wanakamia mechi. Wanapokutana na Simba na Yanga utawaona wachezaji wao wazuri lakini wakikutana na timu kama Namungo au nyingine huwaoni wachezaji hao," alisema Mayele

Ni kauli ambayo inaendelea kudhihiri baada ya Azam Fc jana kukubali kichapo cha mabao 3-1 dhidi ya Namungo Fc katika uwanja wao wa nyumbani, Azam Complex

Ulikuwa mchezo wa pili mfululizo ambao Azam Fc wanapoteza kwani mchezo uliopita walifungwa na Yanga mabao 3-2

Azam Fc walikuwa bora sana kwenye mchezo dhidi ya Yanga wakitoa upinzani mkali kwa mabingwa hao watetezi lakini jana walionekana kuzidiwa na Namungo

Kipigo hicho kinaweza kumuweka matatani kocha wa timu Youssouf Dabo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.