Roma wanafikiria kumkabidhi mshambuliaji wa Uingereza Tammy Abraham, 26, kwa klabu yake zamani ya Chelsea katika mkataba wa kubadilishana mshambuliaji wa The Blues na Ubelgiji Romelu Lukaku, 30, ambaye yuko kwa mkopo katika klabu hiyo ya Italia. (Mirror)
Real Madrid inapanga kuwasajili mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, kutoka Paris St-Germain na mshambuliaji wa Manchester City na Norway Erling Haaland, 23. Klabu hiyo ya Uhispania inanuia kumsaini mchezaji huyo wakati kandarasi yake itakapokamilika msimu ujao. (El Chiringuito, via 90 min)
Arsenal, Manchester United na Manchester City zote zina nia ya kumsajili beki wa Crystal Palace na Uingereza Marc Guehi, 23. (Goal)
Chelsea itamsaka beki na mshambuliaji katika dirisha la usajili la Januari. (Fabrizio Romano)
Arsenal wako tayari kumuuza kipa wa England Aaron Ramsdale msimu ujao baada ya kubadili nia yao kuhusu mustakabali wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Football Insider)
Kiungo wa kati wa Fluminense Mbrazil Andre Trindade, 22, anasema alikataa kuhama msimu wa joto, huku Liverpool na Arsenal zikiwa na nia ya kusaidia timu yake kushinda Copa Libertadores. (90 min)
Liverpool wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Bayern Munich Mjerumani Jamal Musiala, 20, ambaye hajaridhishwa na muda anaopewa kucheza na anachukuliaLigi ya Premia kama mahali pa kuvutia. (Mirror)
Aston Villa wanajiandaa kuanza mazungumzo ya kandarasi na kiungo wa Brazil Douglas Luiz, 25, ambaye Arsenal wanamhusudu. (Football Insider)
Manchester United wanavutiwa na mchezaji wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23 na beki wa Nice Jean-Clair Todibo. (Fabrizio Romano)
Arsenal na Tottenham wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney, 27, lakini hawako tayari kulipa dau la pauni milioni 61. (Fichajes - kwa Kihispania)
Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United na Uingereza Jesse Lingard anatafuta klabu mpya kwa sababu Al-Ettifaq hawana nafasi katika kikosi chao. (Star)
BBC