Mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay na Gremio Luis Suarez, 36, anatazamiwa kujiunga na Inter Miami 2024 ambako ataungana na wachezaji wenzake wa zamani wa Barcelona kama vile Lionel Messi, Sergio Busquets na Jordi Alba. (El Pais - kwa Kihispania)
Chelsea na Arsenal wanawania ya kumsajili Ivan Toney baada ya Brentford kuthibitisha kuwa watamuuza mshambuliaji huyo wa England mwenye umri wa miaka 27 kwa bei inayofaa. (Express)
The Bees wanamthamini Toney kwa pauni milioni 100 lakini wananuia kusalia nayea hadi mwisho wa msimu. (Sky Sports)
Manchester United wanaendelea kutuma maskauti kumfuatilia mlinda mlango wa Ureno Diogo Costa, 24, ambaye wamekuwa wakimnyatia kabla ya kumsajili mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Andre Onana. Lakini ataondoka Porto ikiwa United italipa euro milioni 75 za kifungu cha kutolewa. (A Bola - kwa Kireno)
Real Madrid wanamta mchezaji wa kimataifa wa Canada Alphonso Davies, 22, na wana uhakika wa kukubaliana na klabu yake ya sasa ya Bayern Munich ili kumleta kwenye La Liga msimu ujao. (Relevo - kwa Kihispania)
Arsenal wanapanga kumnunua mshambuliajiwa Slovenia Benjamin Sesko, 20, ambaye aliikataa Manchester United msimu uliopita na badala yake akajiunga na RB Leipzig. (Mirror)
Mkurugenzi wa michezo wa Inter Milan Piero Ausilio amemshutumu mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku kwa utovu wa "nidhamu" kwa kuanzisha mazungumzo na Juventus huku majadiliano kati ya Chelsea na Inter yakiendelea na mchezaji huyo wa miaka 30 hatimaye kujiunga na Roma kwa mkopo. (Mail)
Everton tayari wanataka kumsajili winga wa Leeds United Jack Harrison, 26, kwa mkataba wa kudumu. (Teamtalk)
Manchester United wanavutiwa na beki wa Galatasaray na Ufaransa Sacha Boey, 23, huku Arsenal, Brighton na Burnley pia wakimnyatia. (Mail)
Kocha wa zamani wa Brighton Graham Potter huenda akawa meneja ajaye wa Uswidi baada ya tetesi kuashiria Manchester United wanataka achukue nafasi ya Erik ten Hag. (Mirror)
Real Madrid 'hawana nia' ya kumruhusu kiungo wa Ufaransa Aurelien Tchouameni kuondoka katika klabu hiyo huku Arsenal na Liverpool wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23. (90 Min)
BBC



