Wydad Athletic imejiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa kwanza wa michuano ya African Football League baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mamelodi Sundowns katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa fainali uliopigwa huko Morocco jana
Mabao ya Wydad yalifungwa na Rivaldo Coetzee dakika ya 41 na kipindi cha pili lilifungawa na Anas Serrhat huku Mamelodi wakipata bao dakika ya 74 na Abdelmounaim Boutouil.
Mechi ya marudiano itaamua bingwa wa kwanza AFL Novemba 12 katika dimba la Lucas Masterpieces Moripe, Afrika Kusini
Ni wazi mechi ya pili itakuwa ngumu zaidi Mamelodi wakiwa na kumbukumbu ya msimu uliopita ambapo waliondoshwa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika hatua ya nusu fainali baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Wydad katika uwanja wao wa nyumbani
Timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa Morocco



