Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union ambao utapigwa kesho Jumatano katika uwanja wa Mkwakwani
Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mkoani Tanga leo, Gamondi alisema licha ya ugumu wa ratiba, wamejipanga kushinda mchezo huo
Gamondi amesema kikosi chake kilipata muda mchache wa kufanya mazoezi ya kurejesha utimamu wa mwili baada ya mchezo dhidi ya Simba na baadae kusafiri kuelekea Tanga
Leo watafanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Mkwakwani tayari kwa mchezo huo ambao wanafahamu umuhimu wake
"Sina mengi ya kuzungumza kuelekea mchezo wetu wa kesho dhidi ya Coastal Union kwasababu ya muda, jana tumetumia siku yetu kwa ajili ya kurudisha miili sawa na kusafiri kuja Tanga. Na leo tutakuwa na mazoezi kidogo jioni hayo ndio ninayoweza kusema kwa sasa"
"Michezo inayokuwa kwenye siku za karibu kwenye ligi ina changamoto hasa unapotoka kwenye mechi ngumu na kusafiri lakini Wachezaji wetu wako tayari na wote tunajua umuhimu wa mchezo wa kesho," alisema Gamondi