Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mchezo mmoja unatarajiwa kupigwa katika uwanja wa Mkwakwani
Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga watakuwa wageni wa Coastal Union katika mchezo unaosubiriwa kwa hamu na wakazi wa Tanga na maeneo ya jirani
Baada ya ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya watani zao Simba, Wananchi wanawania alama tatu nyingine mbele ya Wagosi wa Kaya
Hata hivyo hautakuwa mchezo mwepesi kwani Coastal Union hawajawahi kuwa wanyonge walipokutana na Yanga katika uwanja wa Mkwakwani
Coastal Union wamekuwa na mwenendo usioridhisha msimu huu wakishinda mchezo mmoja tu katika mechi nane walizocheza msimu huu
Pengne leo watahitaji kupambana zaidi ili kuweza kupata matokeo mazuri katika mchezo huo



