Coastal Union vs Yanga hapatoshi Mkwakwani leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th November 2023


Coastal Union vs Yanga hapatoshi Mkwakwani leo

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mchezo mmoja unatarajiwa kupigwa katika uwanja wa Mkwakwani

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga watakuwa wageni wa Coastal Union katika mchezo unaosubiriwa kwa hamu na wakazi wa Tanga na maeneo ya jirani

Baada ya ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya watani zao Simba, Wananchi wanawania alama tatu nyingine mbele ya Wagosi wa Kaya

Hata hivyo hautakuwa mchezo mwepesi kwani Coastal Union hawajawahi kuwa wanyonge walipokutana na Yanga katika uwanja wa Mkwakwani

Coastal Union wamekuwa na mwenendo usioridhisha msimu huu wakishinda mchezo mmoja tu katika mechi nane walizocheza msimu huu

Pengne leo watahitaji kupambana zaidi ili kuweza kupata matokeo mazuri katika mchezo huo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.